KARIBU TENA

KARIBU TENA

Sunday, October 13, 2013

Bonnah Education Trust Fund ikidhaminiwa na kampuni ya Simu ya mkonon Tigo yafanya uzinduzi wa mfuko wa elimu wa aina yake.


Mkurugenzi wa Bonnah Education Trust fund Bi Bonnah Kaluwa  aelezea kufurahishwa na mafanikio ya uzinduzi wa mfuko wa kusaidia watoto wasiyokuwa na uwezo wa kulipa ada waliyofaulu kuingia kidato cha kwanza iliyofadhiliwa na Kampuni ya simu ya mkononi ya nchini Tanzania Tigo


Baadhi ya washiriki wa maonyesho ya mavazi wakiwa jukwani na ujumbe wa elimu kwa jamii kama unavyoonekana katika eneo la Mlimani City jijini Dar es Salaam.


Mkurugenzi mtendaji wa Bonnah Education Trust Fund Katikati akiwa na washiriki wa maonyesho ya mavazi jana mlin City jijini Dar es salaam

Mkurugenzi Bonnah Akiwa na Vijana wa maonyesho ya sarakasi waliyokuwa wakinogesha uzinduzi wa mfuko huo wa kuhamasisha kuchangia elimu.


Kushoto ni Bi Regina Ogwao katikati ni mkurugenzi wa Bonnah Education Trust Fund Bonnah Kaluwa nakulia ni Mwenyeki wa umoja wa vijana wa CCM Kata ya Kipawa Saidi Mkuwa Mlimani City Jijini Dar es salaam.


baadhi ya wadau wa Bonna Education Trust Fund wakijadiliana Jambo na mkurugenzi wa Bonnah Kaluwa

Akizungumza na Bloga hii mkurugenzi mtendaji wa Bonnah Education Trust Fund, na Diwani wa kata ya Kipawa jijini Dar Es salaam Mheshimiwa Bonnah Kaluwa alisema kuwa, uzinduzi huo umeambatana na maonyesho ya mavazi yaliyoanzia mnazi mmoja hadi mlimani City jijini Dar es Salaam.


Uzinduzi huo ulipambwa michezo mbalimbali ikiwemo sarakasi, maonyesho ya mavazi, pamoja na mabango mbalimbali yaliyokuwa na ujumbe wa elimu.

Washiriki katika maonyesho hayo wameelezea kufurahishwa kwao na kitendo cha Mheshimiwa Bonnah Kaluwa,kutambua umuhimu wa elimu katika familia masikini na kuamua kuwasaidia.

No comments:

Post a Comment